
Waasi wa M23
Mkuu wa harakati za kudumisha amani wa Umoja wa mataifa Herve
Ladsous ameliambia baraza la usalama la Umoja huo kwamba waasi wameidhinisha
kile anachokiita kuwa ni utawala wa kimabavu Mashariki mwa Jamhuri ya
Kidemokrasi ya Congo.
Bwana Ladsous amesema waasi wa M23 wanadhibiti idadi kubwa ya maeneo ya
Mashariki mwa Congo na wanawatoza kodi wananchi .Waziri wa Madini wa Congo, ameziandikia nchi za Marekani na Uingereza akizitolea wito kampuni katika nchi hizo ziache kununua madini kutoka Rwanda, ambayo mengi anasema yanachimbwa katika ardhi ya Congo.
Zaidi ya watu 200,000 wameachwa bila makao kufuatia mapigano Mashariki mwa nchi.
Mkutano wa maafisa wa ngazi ya juu watakaojadili mzozo huo unatarajiwa kufanyika katika baraza la usalama la Umoja wa mataifa mjini New York wiki ijayo.
"waasi wa M23 wako katika pembe moja ya mkoa wa Kivu Mashariki ambao unapakana na Rwanda na Uganda'' alisema bwana Ladsous wakati akiwahutubia waandishi wa habari mjini New York.

Waasi wanaotoroka vita
Wakati huohuo, maafisa wa utawala nchini DRC wanataka vikwazo kuwekewa biashara ya madini yanayotoka nchini Rwanda.
Wadadisi wanasema kuwa madini mengi yanayotoka nchini Rwanda huenda yalitoka nchini DRC na kuchimbwa na makundi ya waasi walio na uhusiano na Rwanda.
"namna tunavyoweza kukomesha kabisa mzozo huu ni Rwanda kuwekewa vikwazo vya kibiashara kwa madini yanayotoka nchini humo hadi tutakapoweza kupata suluhu la kudumu kwa mzozo katika mikoa ya Kaskazini na Kusini ma Kivu.'' alisema waziri wa madini wa DRC Martin Kabwelulu. .
No comments:
Post a Comment