
Wachimba migodi wakikabiliana na polisi
Polisi nchini Afrika Kusini wametumia risasi za mipira na gesi
ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wanagoma karibu na mgodi
mmoja unaomilikiwa na kampuni ya Anglo American.
Makabiliano hayo yametokea siku moja baada ya mkataba kuafikiwa kati ya
wachimba migodi wa Marikana na wamiliki wa kampuni ya Lonmin.Wafanyakazi wa kampuni ya Lonmin walisitisha mgomo wao wa wiki sita siku ya Jumanne baada ya kukubali nyongeza ya asilimia 22 ya mishahara.
Migomo hiyo ilisambaa hadi katika migodi mingine nchini humo. Afrika Kusini ni mojawapo ya nchi zinazozalisha madini mengi duniani.
Mnamo siku ya Jumatatu rais Jacob Zuma alisema kuwa migomo katika sekta ya madini ililetea nchi hiyo hasara ya zaidi ya dola nusu milioni.
Migomo ilianza nchini humo baada ya kampuni ya madini ya Anglo American Platinum (amplats),kampuni kubwa zaidi ya madini ya Platinum duniani kufungua kiwanda chake baada ya kufungwa wiki jana kufuatia migomo hiyo.
Msemaji wa kampuni ya Amplats, Mpumi Sithole alisema kuwa migodi ya Rustenburg,ambacho ni kitovu cha uchimbaji migodi nchini humo, Kaskazini Mashariki mwa Johannesburg uliendelea na kazi kama kawaida.
No comments:
Post a Comment